CHAMA CHA MAPINDUZI
UMOJA NI USHINDI, AMANI NA MAENDELEO ...!!!

Thursday, October 17, 2013

RAIS KIKWETE AKUTANA NA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KUJADILI RASIMU YA KATIBA

Mhe.Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya Pamoja na Viongozi wa Vyama vya upinzani.Kutoka kushoto: Isaack Cheyo - UDP, James Mbatia - NCCR Mageuzi, Professa Ibrahim Lipumba - CUF, Freeman Mbowe -  CHADEMA, Philip Mangula  - CCM, na Bi. Nancy Mrikaria  - TLP.

Tarehe 15 Oktoba 2013 , Mhe, Rais Jakaya Kikwete alifanya mkutano na viongozi wa vyama vya siasa nchini vyenye uwakilishi bungeni. Mkutano huo uliofanyika Ikulu, Dar-es-Salaam ulihudhuriwa na Mhe. Freeman  Mbowe (Mwenyekiti - CHADEMA),  Mhe. Profesa Ibrahim Lipumba (Mwenyekiti - CUF), Mhe. James Mbatia (Mwenyekiti - NCCR-Mageuzi), Mhe. Nancy Mrikaria ( aliyemwakilisha Mwenyekiti wa TLP, Mhe. Augustine Mrema), Mhe. Isaack Cheyo (aliyemwakilisha Mwenyekiti wa UDP, Mhe. John Cheyo) na Mhe. Philip Mangula (Makamu Mwenyekiti - CCM)

Pia wengine waliohudhuria ni pamoja na Mhe. William Lukuvi (Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge), Mhe. Steven Wassira (Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu), Mhe. Mathias Chikawe (Waziri wa Katiba na Sheria), waheshimiwa Tundu Lissu na John Mnyika kutoka  CHADEMA, Bw. Martin Mng'ong'o kutoka NCCR-Mageuzi, pamoja na Mhe. H. Mnyaa na Bwana Julius Mtatiro kutoka CUF.



Mhe. Rais alikubaliana na viongozi hao mambo yafuatayo:
Kwanza, kwamba vyama vyote vya siasa nchini vyenye mawazo, maoni na mapendekezo ya kuboresha Sheria ya Kurekebisha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba viwasilishe mapendekezo yao haraka Serikalini ili itafutwe namna ya kuyashirikisha mapendekezo hayo katika marekebisho ya Sheria hiyo.

Pili, kwamba vyama vya siasa nchini, kama wadau muhimu katika mchakato wa Katiba mpya, viangalie namna ya kukutana na kujenga mfumo wa mawasiliano na maridhiano kwa pamoja vitakavyosukuma mbele mchakato huo kwa maslahi mapana ya nchi yetu na mustakabali wa taifa. Hivyo basi, Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) kilipewa jukumu la kuratibu jambo hilo ikiwa ni pamoja na kuandaa mkutano wa vyama hivyo na wadau wengine nchini.

Wakati mkutano ukiendelea Ikulu, Dar-es-Salaam

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Vyama vya siasa na wasaidizi wao waandamizi.Kutoka mbele kushoto ni: Isaack Cheyo - UDP, James Mbatia - NCCR Mageuzi, Professa Ibrahim Lipumba - CUF, Mhe.Freeman Mbowe - CHADEMA, Philip Mangula - CCM, na Bi. Nancy Mrikaria. Kutoka nyuma kushoto ni: Julius Mtatiro - CUF, Tundu Lissu - CHADEMA, Martin Mng’ong’o - NCCR Mageuzi, William Lukuvi - (Waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Uratibu na Bunge), Habib Mnyaa - CUF, John Mnyika - CHADEMA, Steven Wassira - (Waziri wa nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu) na Mathias Chikawe (Waziri wa Katiba na Sheria).

Video fupi ya Mhe. Rais Jakaya Kikwete akiwa na Viongozi wa vyama vya siasa na wasaidizi wao, Ikulu - Dar-es-Salaam.



IMETOLEWA NA UONGOZI, TAWI LA CCM MOSCOW - URUSI

No comments: