CHAMA CHA MAPINDUZI
UMOJA NI USHINDI, AMANI NA MAENDELEO ...!!!

Monday, December 9, 2013

SALAMU ZA UHURU KWA WATANZANIA WOTE TOKA CHAMA CHA MAPINDUZI TAWI LA MOSCOW - URUSI

Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akiinua bango kuashiria kupatikana kwa Uhuru wa Tanganyika
Wanachama wa Chama Chama Mapinduzi tawi la MOSCOW nchini URUSI kwa kushirikiana na viongozi wao kwa pamoja wanapenda kutumia fursa hii adhimu kutoa salamu za pongezi kwa watanzania wote popote pale walipo duniani katika sherehe za maadhimisho ya siku ya uhuru wa Tanganyika (Tanzania bara kwa sasa) uliopatikana tarehe 09.12.1961.

Waziri Mkuu wa kwanza wa Tanganyika huru,
Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Akitoa salamu hizo mwenyekiti wa tawi hilo Dkt. Alfred Kamuzora alisema hii ni fursa nyingine ya watanzania kuungana kwa pamoja katika kuadhimisha siku hii ambayo ilipiganiwa ili kulipatia uhuru taifa letu.

Aidha aliongeza kuwa watanzania inabidi kuenzi matunda ya uhuru tulioupata hasa kwa kuzingatia njia ambayo ilitumika kupata uhuru ambayo haikuwa ya umwagaji damu hivyo ni wajibu wetu kuilinda amani ambayo waasisi wetu waliipigania kwa hali na mali ikiwa ni ishara ya kuthamini juhudi zao.

Hayati Meja Alexander Nyirenda akipandisha Mwenge wa Uhuru
kwenye kilele cha mlima Kilimanjaro
usiku ule wa mkesha wa siku ya Uhuru wa Tanganyika
Dkt. Kamuzora alisema kuwa miaka 52  ya uhuru bila mapigano ni jambo la kujivunia sana hivyo ni wajibu wa kila mtanzania kuilinda na kuitetea nchi yake popote pale dunia na kuzidi kuiletea sifa nchi  yetu ambayo inasifika kwa Amani na upendo dunia.
Akimalizia kutoa salamu hizo Dkt. Kamuzora pia alisisitiza watanzania tuzidi kuliombea taifa letu liwe na amani zaidi.

IMETOLEWA NA UONGOZI WA CCM TAWI LA MOSCOW - URUSI

No comments: